Tuesday, March 26, 2013

MICROSOFT KIKAANGONI TENA




Wawakilishi wa watumiaji wa program za wazi chanzo wa Hispania, wamefungua kesi dhidi Kampuni kubwa ya mambo ya kompyuta ya Microsoft katika mahakama ya Umoja wa nchi za Ulaya siku chache baada ya Kampuni hiyo kutozwa faini ya dola milioni 729, kwa kushindwa kuwapa wateja wake uchaguzi wa brouza wanazotaka kutumia.


Wawakilishi hao Hispalinux wamesema kuwa Microsoft wanawabania washindwe kuweka program za Linux kwenye kompyuta zilizowekwa Windows wakati zinauzwa, hali inayowapa shida na usumbufu sana katika matumizi ya kompyuta.


Mwanasheria na kiongozi wa Hispalinux  Bwana Jose Maria Lancho amesema kuwa amefungua mashtaka katika tawi la  mahakama hiyo la Madrid.