Tuesday, April 23, 2013

PAMOJA NA UCHUMI KUPANDA, UMASIKI WAONGEZEKA TANZANIA

Ripoti ya hali ya uchumi duniani imeonesha kuwa idadi ya watu wanaoishi katika umaskini uliopindukia imeongezeka zaidi, huku jirani zetu wa Kenya na Uganda wakiwa wamepiga hatua zaidi katika kupunguza idadi ya watu wanaoishi katika umaskini wa kipato.
Kwa mujibu wa Ripoti ya World Bank iliyoripotiwa kwenye mtandao na Global Monitoring Report 2013, Watu wanaoishi katika umaskini wa kupindukia (wa kipato) ni 38.01% kwa Uganda, 43.37% kwa Kenya na Tanzania ni 67.87%.

Hata hivyo, kwa kuwa tuko katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, na hivi karibuni Rwanda na Burundi wamejiunga nasi kwenye Jumuiya hiyo, tunaweza kujifariji kuwa sisi si wa mwisho Afrika Mashariki, kwani tunaizidi Burundi ambayo 81.32% wanaishi kwenye umaskini uliokithiri (wa kipato). Nchi nyingine ndogo, isiyo na bandari na iliyotoka kwenye matatizo ya mauaji ya kimbari na vita, Rwanda, ina asilimia ndogo zaidi ya maskini kulinganisha na Tanzania, ambapo 63.17% ya Wanyarwanda wanaishi katika hali ya umaskini.