Tuesday, March 26, 2013

FACEBOOK WAONGEZA KITUMIZI

 Facebook imetangaza kuwa itaongeza kitumizi kingine kwenye page za facebook kitakachowawezesha watu kujibu komenti za watu.
Baada ya majaribio ya muda mrefu, wameona ni vyema wakaweka ‘reply’ kwenye komenti ili mtu aweze kuijibu komenti anayoitaka siku nyingi baada ya komenti kutundikwa.
Pia facebook imeamua kuwa mazungumzo yanayoendelea kuchangiwa sana yatakuwa yanakaa juu ili watembeleaji waweze kujua nini kipo hot kwenye page.
Hata hivyo, vitumizi hivyo kwa sasa vitakuwa vikipatikana kwa watumiaji wa kompyuta za mezani tu.