Wednesday, March 27, 2013

BINADAMU WAFANIKIWA KUTOKA NJE YA MFUMO JUA?

Voy­ag­er 1
Miaka therathini toka chombo cha utafiti wa anga za juu Voy­ag­er 1, kinaweza kuwa kimefaulu kutoka nje ya mfumo jua wetu na kuwa chombo cha kwanza kilichotengenezwa na binadamu kufanikiwa kutoka nje ya mfumo jua, habari za kiutafiti zinasema.
Ingawa wanasayansi wanosimamia mradi huo wa Voyager 1 wanapinga taarifa hizo, gazeti la Geo­phys­i­cal Re­search Let­ters  linakubaliana utafiti huo na kusema kuwa kuna kia dallili chombo hicho kimeshatoka nje ya anga zetu.
Chombo hicho cha NASA kimekuwa kikielekea kwenye kingo za Solar System, Aug. 25 kilituma taarifa za mabadiliko makubwa sana ya miale na mionzi kikiwa zaidi ya maili bilioni 11 kutoka kwenye jua.
Wakati huohuo kilionyesha kuwa mionzi kutoka nje ya solar system ikiwa imeongezeka kwa kiasi kikubwa kuliko wakati wowote toka chombo kiondoke.


“Siku chache zilizopita mionzi ya heliospheric imekuwa mikubwa sana na miale ya cosmic imezidi sana.” Alisema Bill Web­ber, falaki waChuo kikuu cha New Mex­i­co State nchini Marekani.