Jeshi
la majini la Misri limefanikiwa kuwakamata wazamiaji watatu wakitaka kukata
nyaya za mawasiliano zinazokuja mpaka Tanzania.
Kukatika
kwa waya za mawasiliano huko Misri imekuwa tatizo kwani kila zinapounganishwa
hukatika tena. Haijulikani kama ni bahati mbaya au wazamiaji watatu ambao
wamekamatwa na wanamaji wa Misri ndio wakataji wa nyaya hizo.
Baada ya tatizo la kukatika nyaya hizo wiki iliyopita kutatuliwa, utata umekuja baada ya kukamatwa watu hawa, kwani mwanzoni ilidhaniwa kuwa zimekatika kwa bahati mbaya lakini sasa watu wanajiuliza kama watu hawa hawahusiki na ukatikaji uliopita.
Baada ya tatizo la kukatika nyaya hizo wiki iliyopita kutatuliwa, utata umekuja baada ya kukamatwa watu hawa, kwani mwanzoni ilidhaniwa kuwa zimekatika kwa bahati mbaya lakini sasa watu wanajiuliza kama watu hawa hawahusiki na ukatikaji uliopita.
Tatizo
lilianza wiki iliyopita wakati nyaya za SEA-ME-WE 4 (South East Asia–Middle
East–Western Europe 4) zilipokatika jirani na Misri. Kampuni inayosimamia nyaya
hizo ilijikuta kila ikitengeza hukatika tena, mpaka ikaamua kuwahamisha njia
wateja wake ili waendelee kupata huduma kwani nyaya bado zimekatika.
