![]() |
| Mufti Mkuu wa Saudia Sheikh Abdul-Aziz Al-Sheik |
Mufti Mkuu Sheikh Abdul-Aziz
Al-Sheik, akiongea
na viongozi wengine wa kidini wa Saudia Ijumaa hii, alisema kuwa mtandao huo ni
‘baraza la wapenda mizaha’ na ni sehemu ya taarifa zisizo sahihi na za
upotoshaji.
Twitter imekuwa ikitumiwa na vijana wanaharakati kuleta
upinzani nchini Saudia pia hata maofisa wa serikali wamekuwa wakitumia twitter
kupeleka taarifa kwa wananchi.
Tamko hilo la Mufti limekuja siku moja na tamko la imam wa
msikiti mkuu wa Mecca lililosema kuwa
ingawa watu wanahaki ya kujieleza, wawe waangalifu ili kujenga heshima na umoja
wa kitaifa.
