Monday, April 22, 2013

KIZIMBANI KWA KULIPUA MABOMU



Dzhokhar Tsarnaev amefikishwa mahakamani kwa makosa ya kulipua mabomu mbio za marathon za Boston,  na akipatikana na hatia anaweza kunyongwa.

Mwendesha mashtaka Eric Holder alitaja makosa aliyoshtakiwa kijana huyo kuwa ni:

  1. Kosa moja la kula njama na kutumia silaha za maangamizi dhidi ya binadamu na mali ndani ya Marekani na kusababisha vifo.
  2. Kosa moja la kuharibu mali kwa kutumia milipuko ambayo ilisababisha vifo.


Kwa makosa hayo, iwapo atapatikana na hatia anaweza kufungwa maisha au kunyongwa.


Mashtaka hayo alisomewa katika mahakama iliyohamia katika chumba cha hospitali anakolazwa kwa matibabu ya majeraha aliyoyapata wakati akipambana na polisi kabla ya kukamatwa.