Monday, April 22, 2013

SERIKALI YAFUNGA VIWANDA VYA NONDO

Inspekta wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Yona Afrika  akizugumza  na Meneja wa Kiwanda cha nondo cha Metro cha  jijini Dar es Salaam, Onesmo Ngondo mara baada ya TBS  kukifungia kiwanda hicho kwa muda usiojulikana , kutokana na kuzalisha nondo  zisizo na  viwango vya ubora vinavyotakiwa. Picha na Beatrice Moses    

Dar es Salaam, Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limevifungia viwanda viwili vya kuzalisha nondo kwa muda usiojulikana.

Viwanda vilivyofungiwa ni vya Metro Steel Mills kilichoko Vingunguti Dar es Salaam na Quaim Steel Milis kilichopo Chang’ombe wilayani Temeke.

Hatua hiyo imekuja baada ya kubainika kwamba vimekuwa vikizalisha na kuuza nondo zisizo na ubora wa viwango vinavyokubalika na hivyo kuwa tishio kwa watumiaji wa bidhaa hiyo.

Na Beatrice Moses, Mwananchi