Monday, April 8, 2013

Windows XP kufutwa?



Pamoja na kuwa Windows 8 haijachanganya vya kutosha, Microsoft imeamua kuiondoa kati matumizi Windows XP ambayo imedumu kwa miaka 11 na bado watu wanaendelea kuitumia, katika juhudi za kuwafanya watu wahamie kwenye OS mpya.

Microsoft imefikia uamuzi huo ambapo itakapofika tarehe  April 8, 2014, hakutakuwa na  updates wala ulinzi kutoka Microsoft kwa watumiaji wa XP hali itakayowafanya watumiaji wa XP kuhamia Windows 7 au 8 bila kutaka.
Kutokana na takwimu za Net Applications mwezi wa 2013, Windows XP, mpaka hivi sasa inatumiwa na asilimia 38 ya kompyuta zote duniani na Microsoft watakuwa na wakati mgumu kuiondoa katika matumizi OS hiyo inayopendwa sana duniani.

Wakiwa wamekatishwa tama na ufanisi wa Windows 8, watumiaji wengi  wameonyesha nia zao kuendelea kuitumia XP pamoja na onyo la Microsoft kuwa watahatarisha data zao na kuzifanya kompyuta zao kuwa wahanga wa mashabulizi ya hackers.