Saturday, May 21, 2011

UNAMILIKI IPAD?

Unajua kuwa Ipad pamoja na kutumika sana kwa burudani na 

mawasiliano, ni kifaa muhimu sana cha kielimu?

 

Mtandao wa wikipedia unataarifu kuwa Ipad wakati ikitoka kwa 

mara ya kwanza, zaidi asilimia 80 ya vitabu vilivyowekwa humo

vilikuwa ni vya elimu kwa watoto.

 

Pia inaripoti kuwa Ipad ni kifaa kinachotumika sana kwa watoto 

wanaosomea nyumbani ambapo vyuo vikuu vingi huko Marekani 

hukodisha kwa wanafunzi wake ili watumie kama visaidizi vya 

masomo.

 

Wakati huohuo Ipad zimesaidi watoto wenye ugonjwa wa autism 

kujifunza kuwasiliana na kujichanganya kwenye jamii kwa urahisi 

sana.