Tuesday, April 2, 2013

POLISI WA NEW YORK (NYPD) WATAADHARISHWA MATUMIZI YA FACEBOOK



Idara ya polisi ya New York imeanza kuwaelekeza maaskari na maofisa wa jeshi hilo matumizi mazuri ya Facebook na mitandao mingine ya kijamii ili kulinda hadhi ya jeshi hilo.

Maelekezo hayo yalikuja kama amri ya kuwataka waangalie wanachotundika kwenye mitandao na kuwahimiza wasiweke wazi kuwa wao ni askari.

“Askari lazima aonyeshe uwezo wa kufanya maamuzi na aonyeshe weredi wa kazi anapokuwa kazini.” Kilisema kimemo hicho. Pia kilionya “Kurasa za mitandao ya kijamii inaweza kutumiwa dhidi yao na kuharibu sifa ya Jeshi, kuingilia utendaji kazi, kuingilia upelelezi wa kesi na kuathiri ajira za askari.” 





Muongozo unawakataza maaskari kutundika picha zao wakiwa na yunifom isipokuwa kama walikuwa kwenye sherehe za kupokea tuzo au kupanda vyeo bila ruhusa ya Jeshi. Askari ataadhibiwa asipotimiza hayo.