Wakiwa hawajaridhishwa na magazilioni ya simu za Galaxy ambazo wameshauza,
Samsung inaendeleza mapambano katika vita kubwa ya kibiashara inayoendelea kwa
kuingia ubia wa mauzo na kampuni ya Best Buy Co., Inc.
Katika ubia huo Best Buy imekubali kuweka viduka vitakavyouza
bidhaa za Samsung katika maduka ya 1400 ya Best Buy yaliyotawanyika sehemu
mbalimbali duniani pamoja na maduka 900 yanayotarajiwa kufunguliwa hivi
karibuni.
Best Buy Co., Inc ni kampuni ya kimataifa ya Marekani
inayojiusisha na uuzaji wa bidhaa za kielektroniki yenye makao makuu Richfield,
Minnesota, na ina matawi pamoja na Puerto Rico, Mexico, Canada and China.
Katika viduka hivyo vitakavyouza bidhaa za Samsung kama simu
na vifaa vyake, Smart TVs na tablets, vitakuwa vikuhudumiwa na wahudumu
walioajiliwa na Samsung ilil kumfanya mnunuzi
aone nini Samsung wanaweza kumpa kwa kiwango cha kumridhisha roho.
Sijui Apple na Microsoft watakopi na kupest staili hii ya
Samsung?
