IBM imezindua teknolojia mpya ya
kuchanganua data kwa upesi sana kuliko ilivyokuwa mwanzo kwa kutumia teknolojia
ya Hadoop na kifaa cha PureData katika mkutano na waandishi wa habari huko San Jose, Califonia, Jumatano iliyopita.
Teknolojia hii itasababisha uchanganuaji wa data uwe wa kasi na zitachanganuliwa
kwa kiwango kikubwa sana na kwa ufanisi mkubwa.
Kwa malengo ya muda mrefu, IBM
imepanga kuwasaidia wateja wake kuepuka tatizo la kugubikwa na mrundikano wa
data za aina mbalimbali kwa kuwatafutia njia za kupambana mapambano
yatakayoleta majibu mazuri zaidi na ufanisi utakaowapelekea kufanya kazi nzuri
nyingi zaidi, alisema Bob Picciano, general manager wa information management ya
IBM Software. “Ndio sababu vifaa vinatakiwa viwe na kasi na uwezo wa kufanya
kazi kubwa sana na viwe rahisi kuvitumia.”

