![]() |
| Bosi wa Touch Bionics, Ian Steven |
Kampuni ya Touch Bionics yenye
makazi yake nchini Scotland, inayoongozwa na Ian Stevens imetangaza kuwa
imefanikiwa kutengeneza mkono wa bandia wenye uwezo mkubwa zaidi kufanya
shughuri za kilasiku za kibinadamu.
Viungo vya bandia ambavyo
vinaunganishwa na mfumo wa neva uliobaki katika mlemavu, hutengenezwa kwa
ushindani mkubwa na makampuni kama Otto Bock ya Ujerumani, RSL Steeper, Touch
Bionics na mengineyo yamefanikiwa kutengeneza viungo vya hali ya juu sana kama
vile vinavyoonekana katika sinema za science fiction ambapo kampuni ya Touch
Basics ilianza biashara hiyo mwaka 2007 ambapo walitengeneza mkono waliouita i-LIMB
Pulse na ukafuatiwa na I-Limb ultra.
Touch Bionics na washindani wake
wamefanikiwa kuvifanya viungo hivyo kufanya kazi kwa kufuata hisia za binadamu.
Baadhi ya mambo yanayoweza kufanya
na mkono huo yanaonyeshwa kwenye klipu hapo juu.

