Tuesday, April 23, 2013
MBUNGE ATAKA KAMPUNI ZA MAREKANI ZIFUKUZWE
Mbunge wa Kawe Halima Mdee ameitaka serikali kuangalia athari za mbegu zinazotoka nje kwani zina madhara makubwa na kampuni hizo zimepigwa marufuku kuingiza mbegu hizo katika nchi mbalimbali ikiwamo India, Argentina, Peru na Ufaransa.
Baadhi ya madhara ni pamoja na utahaira kwa watoto wanaozaliwa, utegemezi kwa kampuni hizo kwani lazima mkulima anunue mbegu kutoka kwao.
WAMEFAULU KUUNDA FIGO
Watafiti kutoka katika hospitali kuu ya Massachusetts, nchini marekani wamefaulu kuunda figo ya bandia ya panya ambayo imeweza kufanya kazi vizuri inapopandwa kwenye panya.
Wataalamu hao walifanikiwa kutengeneza figo hiyo kwe kutumia figo za binadamu na chembechembe za figo ya panya na ikafanikiwa kufanya kazi vizuri.
Hayo yameelezwa na Mtafiti wa Hospitali hiyo wakati akiongea na mtandao wa Nature Medicine, Dr. Harald C. Ott
Akaongeza kuwa uwezekano wa kutengeneza kwa wingi fogo hizo kwa matumizi ya binadamu utakuwa tayari hivi punde.
RAISI AKUTANA NA VIONGOZI WA MADHEHEBU YA KIKRISTO
Viongozi wa dini wamewataka waumini kote
nchini kulinda amani na umoja uliopo ili nchi isije ikaingia kwenye mgawanyiko
wa kidini na kuleta machafuko hapa Tanzania.
Wito huo umetolewa na viongozi wa dini leo Ikulu ya Dar-Es-Salaam mara baada ya kikao cha pamoja baina ya viongozi wa dini na Rais Jakaya Kikwete.
Viongozi hao wa dini wamefika leo wakiongozwa na Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
Viongozi wengine wametokea Baraza la Kikristo Tanzania (CCT) Seventh Day Advertist (SDA) na Baraza la Pentekoste Tanzania (PCT).
Mkutano huo umeanza kwa Askofu Ngalalekumtwa kusoma tamko lao la pamoja kwa Rais Kikwete ambalo ndilo limetoa muongozo wa mazungumzo hayo ya leo ambayo yamehusu Amani na Usalama wa Taifa na migogoro ya kidini ndani ya jamii.
Mkutano wa viongozi wa dini ya Kikristo Tanzania ni mojawapo ya jitihada za Rais Kikwete kutafuta muafaka na kutafuta utatuzi wa hali ya sintofahamu ambayo inanyemelea nchi yetu katika kipindi hiki.
Wito huo umetolewa na viongozi wa dini leo Ikulu ya Dar-Es-Salaam mara baada ya kikao cha pamoja baina ya viongozi wa dini na Rais Jakaya Kikwete.
Viongozi hao wa dini wamefika leo wakiongozwa na Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
Viongozi wengine wametokea Baraza la Kikristo Tanzania (CCT) Seventh Day Advertist (SDA) na Baraza la Pentekoste Tanzania (PCT).
Mkutano huo umeanza kwa Askofu Ngalalekumtwa kusoma tamko lao la pamoja kwa Rais Kikwete ambalo ndilo limetoa muongozo wa mazungumzo hayo ya leo ambayo yamehusu Amani na Usalama wa Taifa na migogoro ya kidini ndani ya jamii.
Mkutano wa viongozi wa dini ya Kikristo Tanzania ni mojawapo ya jitihada za Rais Kikwete kutafuta muafaka na kutafuta utatuzi wa hali ya sintofahamu ambayo inanyemelea nchi yetu katika kipindi hiki.
PAMOJA NA UCHUMI KUPANDA, UMASIKI WAONGEZEKA TANZANIA
ATHARI ZA UWEKEZAJI?
Monday, April 22, 2013
KIZIMBANI KWA KULIPUA MABOMU
Dzhokhar Tsarnaev amefikishwa mahakamani kwa makosa ya kulipua mabomu mbio za
marathon za Boston, na akipatikana na
hatia anaweza kunyongwa.
Mwendesha mashtaka Eric Holder alitaja
makosa aliyoshtakiwa kijana huyo kuwa ni:
- Kosa moja la kula njama na kutumia
silaha za maangamizi dhidi ya binadamu na mali ndani ya Marekani na kusababisha
vifo.
- Kosa moja la kuharibu mali kwa kutumia milipuko ambayo ilisababisha vifo.
Kwa makosa hayo, iwapo atapatikana
na hatia anaweza kufungwa maisha au kunyongwa.
Mashtaka hayo alisomewa katika mahakama iliyohamia katika chumba cha hospitali anakolazwa kwa matibabu ya majeraha aliyoyapata wakati akipambana na polisi kabla ya kukamatwa.
Subscribe to:
Comments (Atom)





